ULIMWENGU WETU
1. Jina la mola ndo kambi,nami
ninakimbilia,
Ili anipe ulumbi,wa
vina kupangilia,
Kati ya tungo
tutumbi,yangu isije ingia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
2. Kuna wetu ulimwengu,tuliojichagulia,
Una radha kama
kungu,ndugu zangu nawambia,
Kwetu hakuna
ukungu,giza tumelikimbia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
3. Tumerefushwa mikono,mgongo
twajisugua,
Tunajilia vinono,ni
supu kwa vitumbua,
Tunabalikiwa
mno,kila tunapopumua,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
4. Tunairamba asali,hamu inapotujia,
Hatuitafuti
mbali,ndani tumejijazia,
Hatutumii
nauli,radha kuisafilia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
5. Tunakula wali nazi,kwa viungo
miamia,
Tunkula kwa
mchuzi,vizuri unonukia,
Tunashushia kwa
ndizi,tunda tunalotumia
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
6. Twakuta ndani liwazo,moyo unapoumia,
Yakitujaa mawazo,
faraja hukimbilia,
Vitokeapo vikwazo
mola,anatukingia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
7. Ulimwengu wetu pepo,si kufuru
naapia,
Wanaishi kama
popo,humu wasioingia,
Nami nashika
kiapo,humuhumu nitafia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
8. Ulimwengu wa maraha,si peke
niloingia,
Hata bwana
Mafutaha,huku amekimbilia,
Atembea kwa
madaha,Kalindima akimbia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
9. Bwana makame wa Tanga,tunda
kashajivunia,
Mkongwe Jamili
Mwanga,mbona ameshaingia,
Mtekateka
katinga,mama kanichukulia
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
10. Abidala wa msese,kakayo
hajakwambia,
Mboga twaunga
mawese,kwa nyanya na mabamia,
Fanya bidii
unase,vitamu uje jilia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
11. Raisi Mwakitalima,huku kumemnogea,
Kila apatapo
nema,heka ujiongezea,
Waone kina
Ndatama,wanavyojinenepea,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
12. Hakika nusu ya dini,sisi
tumejitwalia,
Kama nanyi
mwatamani,basi ifateni njia,
Mje ingia
kundini,pepo kuikaribia,
Huu ulimwengu wetu,una radha
kemkem.
Mtunzi:Lutufu A. Mbanga(Utu busara)
S.L.P 1 MOROGORO –O655133337-lutufumbanga@gmail.com
No comments:
Post a Comment